Akizungumza katika bunge hilo Mbatia amesema kuwa 
kitendo cha polisi cha kuwapiga raia wasiokuwa na hatia, kuwazalilisha 
waandishi wa habari na kupiga mabomu ya machozi kiasi cha kuwafanya 
watoto wadogo kuhangaika hakikubaliki.
                
              
Amesema polisi wakiendelea kuachwa kufanya vitu 
vya uvunjifu wa Amani Serikali haitatawalika hivyo ili kurejesha amani 
na imani ya wananchi kwa Serikali yao ni vema shughuli zote za Bunge 
zikaahirishwa kupisha mjadala wa hoja hiyo binafsi kwa lengo la 
kuinusuru nchi.
                
              
“Mheshimiwa Spika naliomba bunge lako liahirishe 
shughuli zake ili leo tuweze kujadili suala hili la uvunjifu wa amani 
uliofanywa na  jeshi letu la polisi jijini Dar es Salam jana, wao 
wanasema kuwa wamepewa amri kutoka ngazi za juu tunataka serikali 
ituambie ni nani anayetoa amri hizi za kupiga watu wasiokuwa na hatia 
yeyote, amesema Mbatia.
                
              
Baada ya kuwasilisha hoja hiyo asilimia kubwa ya 
wabunge walisimama juu Kisha  kuunga mkono hoja hiyo lakini Spika 
Makinda akawaomba wakae ili aweze kutoa ufafanuzi kwa mujibu wa kanuni.
                
              
Spika makinda aliwaeleza wabunge hao kuwa suala 
hilo ni nyeti kwa sababu ni la kiusalama, ili kupata ufafanuzi zaidi 
anaiagiza Serikali kufikisha bungeni hapo majibu ya hoja hiyo kesho ili 
wabunge waweze kujadili.
                
              
Baada ya maamuzi hayo ya Spika Makinda kelele 
zikasikika bungeni huku wabunge wakitaka kufanyika kwa mjadala huo leo 
leo, ndipo Spika alipoamua kuahirisha bunge hadi saa kumi jioni.
0 comments:
Post a Comment