WAGENI KUTORUHUSIWA KUMILIKI ARDHI AFRIKA YA KUSINI!!

Rais Jacob Zuma wa Afrika ya Kusini. (Picha na Maktaba)
Rais Jacob Zuma amesema kuwa hakuna Wageni hawatakaoruhusiwa kumiliki ardhi Afrika Kusini, ikiwa ni moja ya  sheria kali zinazopendekezwa na Rais Jacob Zuma.

Bw Zuma amesema kuwaSiku zijazo wageni wataruhusiwa tu kukodi kwa muda mrefu ardhi ya mashamba katika nchi hiyo ya Afrika Kusini.

Mbali na hayo, mtu yeyote anayemiliki zaidi ya hekta 12,000 atalazimishwa kuiuzia serikali ili ipate kugawiwa.

Ardhi bado ni swala linalozusha hamasa nchini humo  ambako karne tatu za ukoloni na ubaguzi wa rangi - zimeacha ardhi nyingi mikononi mwa wachache, hasa wazungu.

Tangu kumalizika kwa ubaguzi wa rangi mwaka 1994, chama tawala cha ANC, kimeshindwa kufikia lengo lake la kugawa theluthi ya ardhi ya kilimo kwa Waafrika, ulipofika mwaka 2014.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment